Pages

Wednesday, November 13, 2013

MWALIKO MWALIKO MWALIKO


CHAMA CHA VIJANA WA KANYIGO WANAOISHI DAR ES SALAAM TANZANIA, KINAPENDA KUWAKARIBISHA KWENYE HAFLA YA KUCHANGIA PESA YA KUNUNU VITABU VYA SHULE ZA MSINGI KATIKA KATA ZA KANYIGO NA KASHENYE ITAKAYOFANYIKA MSASANI BEACH SIKU YA JUMAPILI TAREHE 24.11.2013 KUANZIA SAA 12.30 JIONI.

IKUMBUKWE KUWA ELIMU NI NYENZO MUHIMU SANA KATIKA MAISHA YETU, KAMA MDAU WA ELIMU UNAKARIBISHWA SANA.

MGENI RASMI TAKUWA MBUNGE WA JIMBO LA NKENGE MH, ASUMPTA MSHANA,

WAITU MUNYEGERE NAKANYETO

Tuesday, May 7, 2013

HISTORIA YA VITA YA KAGERA 1978-1979


MAJESHI YA UGANDA YALIVYOINGIA KAGERA

MWAKA 1978, Majeshi dhalimu ya Nduli Idi Amin Dadaa wa Uganga, yalivamia Ardhi ya Tanzania, eneo la Mto Kagera, katika mkoa wa Ziwa Magharibi na kufanya uharibifu mkubwa wa mali na kuua wananchi wa mkoa huo, NYAKASAGANI MASENZA anasimulia kupitia vyanzo mbali mbali vya habari jinsi majeshi hayo yalivyoingia Tanzania na Amin kutangaza rasmi kuwa eneo hilo la Mto Kagera ni sehemu ya Uganda.

DAIMA Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwa ukombozi wa Bara la Afrika, ikiwa miongoni mwa mataifa masikini zaidi duniani, lakini iliyojariwa viongozi wenye hekima, kuanzia muasisi wake Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Rais wa pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete.

Busara za viongozi wa Tanzania zilianza kuonekana mwaka 1961, baada ya Mwalimu Nyerere kuwanasua watanzania kutoka mikononi mwa utawala kandamizi wa wakoloni, wakati huo pia akiwa tayari kuchelewesha Uhuru wa Tanganyika ili nchi zingine zilizokuwa kwenye mchakato wa uhuru zipate Uhuru siku moja na Tanganyika.

Msimamo dhabiti Mwalimu Nyerere, uliweza kujenga Tanzania imara na kuifanya kuwa Taifa kimbilio la vikundi na vyama vya wapigania uhuru Kusini mwa Afrika, ambao walipewa hifadhi ya kudumu na kutumia ardhi ya Tanzania kuwa sehemu ya mapambano ya kudai uhuru wao, ambao waliupata kupitia mgongo wa Tanzania.

Viongozi kama Hayati Edward Mondolane, Samora Macheli wa Msumbiji, Nelson Mandela wa Afrika Kusini, Yoweri Mseveni wa Uganda, ni sehemu ya viongozi waliopitia mikononi mwa Mwalimu Nyerere wakati wakipigana nchi zao zikombolewe.

Watanzania walianza kuingiwa na wasiwasi mwaka 1971, wakati Nduli Idi Amin Dada alivyoasi na kuchukuwa madaraka ya Uganda kwa nguvu baada kuungusha utawala halali wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Hayati Milton Obote na kutangaza kuitawala nchi hiyo kijeshi.

Mwanzo wa utawala wake waganda pamoja na mataifa mengine walidanganyika, wakawa na matumaini makubwa juu ya kiongozi huyo wa kijeshi, kutokana na ahadi zake nyingi kwamba yeye ataitala uganda na kuhakikisha eneo lililoko Tanzania, sehemu ya mto kagera, katika mkoa wa Ziwa Magharibi litakuwa sehemu ya Uganda.

Mwaka huo huo, Idi Amin alijaribu kutimiza madai yake kwa kuishambulia sehemu hiyo ya Mto Kagera, lakini watanzania walikuwa imara katika kulinda ardhi yao sehemu hiyo akashindwa, baada ya majeshi yake kurudishwa nyuma na majeshi hodari ya Tanzania.

Pamoja na majeshi yake kurudishwa nyuma, Fashiti huyo aliyejitangaza kuwa Rais wa maisha wa Uganda, akiwapongeza wapiganaji wake kwa kurudishwa nyuma huku akiwasifia kupata jeraha kidogo kutoka kwa majeshi ya Tanzania.

Baada ya wapiganaji wake kurudishwa nyuma Idi Amin alisema huo ni mwanzo tu, awamu nyingine atatumia silaha nzito zaidi ikiwa pamoja na makombola ya kurushwa kwa ndege na kuwaongezea nguvu askari wa miguu, jambo ambalo liliwafanya waganda kuingiwa na hofu kutokana na utawala huo wa mabavu, baada ya Amin kuanza kuwatilia shaka wananchi na kuwaua hovyo.

Mauaji ya kinyama yakawa kitu cha kawaida katika Uganda, wananchi wengi wasiokuwa na hatia walipoteza maisha, watu mashuhuri kama Jaji Mkuu Benedicti Kiwanuka na Askofu Mkuu Jamal Luwumu, waliteswa na kuuawa chini ya utawala wake.

Aitoa amri kuwa watu wote wanaopinga utawala wake, wapigwe risasi hadhalani, katika kutekeleza moja ya ndoto zake alizodai kuwa ni mazungumzo baina yake na Mwenyezi Mungu, aliwafukuza kutoka Uganda, Waasia wote waliokuwa na pasi za kusafiria za Uingereza na kuwanyanganya mali zao zote.

Baada ya shutuma nyingi za uongo dhidi ya Tanzania, mnamo tarehe 30 )ktoba 1978 Idi Amin aliyaamuru majeshi yake kuvuka mpaka na kulivamia eneo la Tanzania, ambapo watanzania zaidi ya 10,000 wasiokuwa na hatia yaliangamizwa na eneo la kilomita za mraba 1850 zilichukuliwa na majeshi ya Uganda.

Majeshi hayo ya Amin yalilikalia eneo la mto Kagera sehemu ya kyaka na kufanya vitendo vya kinyama kwa kuua wananchi wa mkoa wa Ziwa Magharibi hovyo, kuchoma nyumba, viwanda, kupora mali nyingi na kuzipeleka Uganda.

INAENDELEA

Monday, January 14, 2013

GET TOGETHER EVENT ON 23 FEB 2013

Habari wanachama,

rejea kikao kilichopita, tumekubaliana siku ya 23.02.2013 tutafanya get together party ya mwaka wa jana, ikumbukwe, tulishindwa kufanya hii party ambayo ipo kwa mujibu wa katiba kutokana na mambo kuwa mengi ndani ya kalendar ya chama, kuna mengi sana yatafanyika siku hiyo, msikose kwani ni kosa kikatiba kukosa siku hiyo.

Imetolewa na japhet Mukala

Sunday, February 5, 2012

HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE (1938-1984)

HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE (1938-1984)


Leo Aprili 12,2009 ni miaka 25 tangu afariki Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine. Sokoine alifariki kwa ajali ya gari huko Dakawa nje kidogo ya Mji wa Morogoro,katika barabara kuu ya MOROGORO-DODOMA akiwa anatokea Dodoma kwenye Kikao cha Bunge.
Tutamkumbuka kwa jinsi alivyojishughulisha na kukomesha UFISADI wa wakati ule.

1 Maoni yako:

  1. Ufisadi kwa wakati ule na sasa tutaita Dhuluma.
    Hivi leo tunaweza tukatangaza vita Dhidi ya "wahujumu uchumi na walanguzi?" Hizi ni siasa zilizopitwa na wakati. Siasa zilizorudisha maendeleo ya Tanganyika (au Tanzania). Tushazika siasa za ujamaa na kujitegeme na tumegundua baadaye kwamba fikra sahihi za mwenyekiti wa C.C.M zilikuwa si sahihi kabisa. Juu ya kuwa walikuwa na nia safi lakini tukubali walichemsha! Na baadaye tukafata soko huru kama alivyobashiri bwana Oscar Kambona, ambayo Nyerere na Kawawa waliyapinga.

Monday, December 19, 2011

UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA-MWL NYERERE

Nchi yetu bado changa. Tusione haya kuendeleza taratibu ambazo zinaonekana kuwa zinafaa, na wala
kubadili zile ambazo japokuwa huko nyuma zimetufaa, lakini sasa "zimepitwa na wakati." Ndivyo
tulivyofanya kuhusu mfumo wa chama kimoja; tusiogope kufanya hivyo kuhusu mageuzi ya kuleta
demokrasia zaidi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Inawezekana kwamba demokrasia peke yake ambayo kwa sasa itaendelea kuwa na maana kwa nchi hii
wakati tunasubiri kupata mpinzani mzuri na makini nje ya CCM, ni demokrasia ndani ya CCM.
Wanachama wa CCM wana wajibu wa kukitazama upya chama chao na kuona jinsi ya kuongeza
demokrasia ndani yake. Wajibu huu si kwa chama chao tu, ni wajibu wa uzalendo kwa manufaa ya
Tanzania nzima.
75
WOSIA
Ole wake Tanzania
Tusipoisaidia!
Niwezalo nimefanya:
Kushauri na kuonya.
Nimeonya: Tahadhari!
Nimetoa ushauri:
Nimeshatoka kitini;
Zaidi nifanye nini.
Namlilia Jalia
Atumulikie njia;
Tanzania ailinde,
Waovu wasiivunde.
Nasi tumsaidie
Yote tusiyamwachie!
Amina, tena Amina!
Amina tena na tena!
T A M A T I

Monday, December 12, 2011

Photos: Andre Villas-Boas Roars Again: Chelsea-Manchester City, 2-1 (PHOTOS)


Photos: Andre Villas-Boas Roars Again: Chelsea-Manchester City, 2-1 (PHOTOS)

Despite all the bad press he has been generating these days, Andre Villas-Boas has reason to cheer again.
The Blues were able to end the unbeaten run of Premier League leaders Manchester City who were beaten 2-1 at Stamford Bridge on Monday night despite an early goal from Mario Balotelli.
Balotelli struck just 98 seconds into the game, but Chelsea were level on 34 minutes when Raul Meireles brilliantly volleyed home a timely cross from Daniel Sturridge.
Gael Clichy was sent off on 58 minutes for a second yellow card.  And Frank Lampard's late penalty sealed the victory in favour of Chelsea, marking City's first defeat in this competition.
As of now, City lead the table by just two points ahead of neighbours Manchester United.
Here are some of the key moments from the action:
Chelsea-Manchester City
Manchester City's Mario Baoltelli celebrates his goal against Chelsea during their English Premier League soccer match in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
Chelsea-Manchester City
Chelsea's Jose Bosingwa and Ramires challenge Manchester City's David Silva during their English Premier League soccer match in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
Chelsea-Manchester City
Chelsea's Didier Drogba reacts during their English Premier League soccer match against Manchester City in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
Chelsea-Manchester City
Manchester City's Gael Clichy is sent off by referee Mark Clattenburg during their English Premier League soccer match against Chelsea in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
Chelsea-Manchester City
Chelsea's Frank Lampard shoots and scores a penalty past Manchester City goalkeeper Joe Hart during their English Premier League soccer match in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
Chelsea-Manchester Cit
Chelsea's manager Andre Villas-Boas reacts during their English Premier League soccer match against Manchester City in London.
Source: Reuters Date:12/13/2011
This article is copyrighted by IBTimes.co.uk, the business news leader